Zidane amekasirishwa na hatua ya Real Madrid kushindwa kumsajili Pogba

Kocha wa Real Madrid Zinedine Zidane amekasirishwa na hatua ya viongozi wakuu wa klabu hiyo kushindwa kumsajili Paul Pogba,26, kutoka Manchester United. (Sports)

Neymar ameifahamisha Paris St- Germain kuwa yuko tayari kurudi chini na kuboresha uhusiano wao endapo atakosa nafasi ya kuhamia Barcelona ama Real Madrid kabla dirisha la uhamisho wa wachezaji Ulaya kufungwa msimu huu.( Independent)

Mwenyekiti wa Crystal Palace Steve Parish amesema atamruhusu mshambuliaji wa Ivory Coast forward Wilfried Zaha, 26, kuondoka klabu hiyo msimu ujao wa uhamisho wa wachezaji- ikiwa dau lililotangazwa na Arsenal na Everton litafikiwa. (Daily Mail)

Parma wamekubali mpango wa kumsajili beki wa Manchester United Matteo Darmian kw euro milioni 1.4 (Sky Sports)

Huku hayo yakijiri, mkurugenzi wa kiufundi wa Paris St-Germain Leonardo amesema mabingwa hao wa Ufaransa hawajakaribia kufikia makubaliano na Barcelona kumhusu Neymar. (Marca)

Meneja wa klabu ya Barcelona Ernesto Valverde amesema kuwa amechoshwa na mashauriano yanayozunguka uhamisho wa Neymar kuja klabu hiyo (Standard)

Mkufunzi wa Arsenal Unai Emery amesema kuwa mlango upo wazi kwa kiungo wa kati wa klabu hiyo Mesut Ozil kurejesha hadhi ya mchezaji nyota wa Gunners.(Mirror)

Paris St-Germain wamewatambua wachezaji kiungo wa kati wa Tottenham Christian Ericksen 27, na mshambuliaji wa Juventus Paulo Dybala,25, kama wachezaji wawil8 watakao chukua nasi ya Neyma endapo atahamia Barcelona (Le Parisien kwa kifaransa)

Mshambuliaji wa zamani wa Tottenham Fernando Llorente,34, amekubalia kutia saini mkataba wa miaka miwili na Napoli inayoshiriki Ligi Kuu ya Italia, Serie A (Sky Sports)

-BBC