- Wameoana miezi mitatu iliyopita
- Esma anasema mume wake huyo alikuwa akizungumza na wasichana katika instagram
- Esma ni mama ya watoto wawili
Dadake msanii wa Bongo Diamond Platnumz Esma Platnumz, ametengana na mume wake Msizwa Maulid baada ya ndoa yao kudumu kwa miezi mitatu pekee .
Esma alitumia instagram kutoa ujumbe huo wakati wa maswali na majibu na mashabiki wake . Esma na Msizwa walifunga ndoa julai tarehe 30 mwaka huu na amesema alimua kuachana naye kwa sababu amekuwa akiwatongoza wanawake wengine katika instagram yake .
‘VERY BAD KWA PETIT NILIZOEA SABABU WOTE TUNAJULIKANA ILA KUWA NA MTU ASIYEJULIKANA AKAJULIKANA INSTAGRAM CHANGA MOTO SABABU KUNA WAKATI ANAJISAHAU NA INSTA KULIKO MAISHA YAKE KUNA WAKATI ANAWADM WATU INSTA SOO BAD.’
Esma Platnumz, mama ya watoto wawili awali alikuwa ameolewa na alikubali kuolewa tena na Msizwa kama mke wa tatu .
Akieleza mbona alikubali kuolewa kama mke wa tatu ,Esma amesema alitaka kupata funzo akiongeza ;
‘Ili kujua mambo mengine na kujifunza lazima ujitoe kama kafara’
Uamuzi wake wa kuachana na mumewe ulizua maoni mbali mbali mtandaoni ;
mercy_ramsey Unatarajia kuoa lini tena Niko single Mr Msizwa.
montaner__tz Mzee wa ku dm madem
megaoriginalest Esma kama amechoka kuvumilia. Ameona wacha isiwe taabu
nicelo Karma is a bitch!! That bitch slaps HARD!!!! Ya feel me!! Kwa alichowafanyia wapenzi wa kaka yake wacha aisome namba
new_carrymastory Esma alisema eti huwa unawatumia watu msg DM hii tabia haipendi eti, hivi uliona ile insta story yake ya jana nimeona tu nikupe umbea maana unaniwashaaa
shamimshaaban96 Umeachwa n Esma ndio warudi kwa melo