•Mtangazaji huyo amesema kuwa amekuwa akisumbuliwa na homa kali.
•Oguttu amehimiza Wakenya wote waendelee kuvaa barakoa na kusafisha mikono
Mtangazaji wa habari mashuhuri Lindah Oguttu ametangaza kuwa amepimwa na kupatikana na virusi vya Corona.
Akitoa tangazo hilo kupitia mtandao wa Twitter, Oguttu amesema kuwa amekuwa akisumbuliwa na homa kali.
Mtangazaji huyo amesema kuwa amepoteza hisia ya harufu na ladha.
"Nimepimwa na kupatikana na virusi vya Corona na wacha niwaambie, ile homa inakuja na maradhi haya ni mbaya. Harufu hakuna! Tilapia kutoka Yurop inaonja kama sponji(Mwiko). Mwili yote inauma. Tumeni Kaluma,Rob, supu n.k. Naumia," Alisema Oguttu.
Oguttu amehimiza Wakenya wote waendelee kuvaa barakoa na kusafisha mikono.
Just tested positive for COVID 19 and let me tell you Maina, the fever this thing comes with is crazy. Smell, taste onge😳. Tilapia from Yurop tastes like sponge (abomination). Mwili yote nauma. You people send Kaluma, Rob, soup etc. Naumia. But seriously guys, mask up, sanitize.
— Lindah Oguttu (@lindahoguttu) July 29, 2021
Wanamitandao wameendelea kumtakia afueni ya haraka mtangazaji huyo.