Sijawahi nyanyasa mtu kingono,Diana amwambie mumewe ukweli-Willy Paul azungumzia madai ya ubakaji ya Diana Marua na Miss P

Muhtasari
  • Pia Willy Paul a.k.a Pozze hatimaye amejitetea kutokana na madai ya aliyekuwa msanii wake Miss p
Image: INSTAGRAM// WILLY PAUL

Diana Marua ambaye sasa anajulikana kama Diana B katika tasnia ya muziki ameibuka na shutuma kali dhidi ya mwanamuziki mwenzake Willy Paul.

Amefunguka kuhusu kuvamiwa na machozi yake yangefichua kuwa kweli kilichotokea kilikuwa na athari kubwa katika maisha yake na amekuwa kimya kwa muda mrefu.

Hata hivyo, Willy  amejibu madai hayo kwa kuwashutumu Bahati kwa kutaka kumharibia jina akisema ni kwa sababu wimbo wake mpya'my woman' ambao umekuwa ukivuma mitandaoni.

Ameendelea kwa kusema kuwa alikuwa na jambo na Diana zamani na haikuwa kitu kigumu kwa hivyo anapaswa kujitokeza na kumwambia ukweli mumewe, kwa sababu ilidumu chini ya masaa 24.

Pia Willy Paul a.k.a Pozze hatimaye amejitetea kutokana na madai ya aliyekuwa msanii wake Miss p.

Miss P alidai kuwa Pozze alikuwa mnyanyasaji kwa njia ambayo alimshinda na kuwa na njia yake pamoja naye.

Pozze alienda kortini na kupata amri ya kuwa mahojiano ya video hiyo iolewe mitandaoni, Hata hivyo, leo asubuhi ameangazia madai ya unyanyasaji wa kijinsia.

"Miezi michache iliyopita, mwanamke ambaye nilimpenda sana alidai kwamba nilimnyanyasa kingono kwa sababu ya tofauti tulizokuwa nazo kuhusu baadhi ya kazi tunazofanya pamoja studio.

Hilo lilikuwa jiwe la kwanza lililofanikiwa kuvunja ngozi yangu nene. Nilihisi kusalitiwa nilipata msongo wa mawazo na bado niko chini ya dawa. Ninahisi mazingira magumu. Suala hilo liko mahakamani na siwezi kulizungumzia zaidi."

Je Pozze amekuwa kama msanii R.Kelly ambaye alishtumiwa na wanawake kadhaa kwa unyanyasaji wa ngono, kama wanavyodai mashabiki wake?

Hii si mara ya kwanza kwa Poze kupokea tuhuma za namna hii na Diama amedhamiria kuendelea na kesi dhidi yake.

Aidha Pozze amesema kwamba ameachia kila kitu Mungu.