• Yamoto band kimetangaza kurejea kwa kishindo kikubwa, hii ni baada ya kusambaratika kwake.
•Amesema amesajili wasanii wapya ambao wataleta mhemko wa aina yake na kuzuzua nyoyo za mashabiki wa Bongo.
• ametangaza rasmi kuwa kikundi hicho mwaka huu 2022 kinarudi kuwapa burudani mashabiki wake.
Kikundi cha wanamuziki kutoka nchi ya Tanzania cha Yamoto band kimetangaza kurejea kwa kishindo kikubwa baada ya kusambaratika miaka kadhaa iliyopita.
Mkubwa Fella kupitia kituo kimoja cha radio nchini Tanzania ametangaza rasmi kuwa kikundi hicho mwaka huu 2022 kinarudi kuwapa burudani mashabiki wake.
Kulingana naye bendi hio ilisambaratika kufuatia wanachama wake kuanza kurekodi muziki nje ya kikundi hicho, jambo ambalo lilikuwa kinyume na mikataba yao.
Wasanii walioanzisha kikundi hicho, walikuwa Aslay, mbosso, Enock Bella na meneja akiwa Mkubwa Fella.
Mkubwa Fella amesema mwaka 2022 anataka kuhakikisha kikundi hicho kimerudi kwa kishindo na mashabiki wake watarajie muziki waliokosa wakati kikundi hicho kilingia mitini.
Fella ambaye pia ni mbunge alisema kwamba, ifikiapo mwezi wa Februari wataachilia kibao chao cha kwanza na hivyo kuomba mashibiki kuwapokea kama kitambo.
Fella ambaye alijulikana kwa ubunifu wake wakati bendi hiyo ilikuwa inatesa anga. amesema amesajili wasanii wapya ambao wataleta mhemko wa aina yake na kuzuzua nyoyo za mashabiki wa Bongo.