Mwanasosholaiti na mfanyabiashara sifika Zari the Boss Lady amejitokeza na kuzungumzia mwanamume aliyeonekana naye kwenye picha moja ambayo imekuwa ikisambazwa mitandaoni.
Kupitia kituo kimoja cha habari cha Uganda, ambacho kilimhoji Zari, alieleza kuwa jamaa aliyekuwa naye kwenye video iliyosambazwa mitandaoni ni rafiki yake na si mpenzi wake kama wanamtandao wanavyodhani.
"ni rafiki yangu huyu,tafadhali acheni kueneza uongo mtandaoni," alisema Zari.
Baada ya meza ya udaku kupiga mbizi ili kupata kina cha uvumi huu ilibainisha jina halisi la jamaa huyo kuwa GK Choppa ambaye ni tajiri sifika Afrika Kusini.
Vilevile, Gk Choppa ameonekana kuchapisha video iliyokuwa ikionyesha akimkaribisha Zari kwenye himaya yake.
Zari,ambaye ni mpenzi wa zamani wa Diamond Platinmuz na Mama wa watoto wawili wa msanii huyo, tangu waachane na Diamond hajakuwa akiposti picha na wanaume isipokuwa wikendi hii ambayo alipakia picha wakiwa na Dk Choppa.