• Mwanamuziki wa nyimbo za Taraab kutoka nchi ya Tanzania, Khadija Kopa ameeleza kuwa yeye ni mkwe wa taifa
• Alisema kwa sasa popote anapotembea anaitwa mkwe wa taifa, kauli ambazo zinazofanya ajivunie kuwa mama wa Zuchu.
Staa wa Taraab kutoka nchi ya Tanzania, Khadija Kopa ameeleza kuwa yeye ni mkwe wa taifa.
Kauli hii imechukuliwa kwa uzito kuzingatia tetesi kwamba Diamond anatoka kimapenzi na mwanamuziki Zuchu.
Khadija Kopa ambaye alikuwa anahojiwa na kituo kimoja cha habari nchini Tanzania, alisema kwamba furaha kubwa kwa kila mzazi, ni kuona watoto wake wakikua kwa madili mema yanayofaa.
Alisema popote anapotembea anaitwa mkwe wa taifa, kauli ambazo zinazofanya ajivunie kuwa mama wa Zuchu.
"Umezaa Mtoto wa kike utakosa aje kuitwa Mkwe, Mimi ni mkwe wa taifa, Nimefunza watoto wangu kwa njia inayofaa kwa hivyo sina shaka kusema anajua jinsi ya kutunza familia," alisema Khadija Kopa.
Khadija, ambaye ni mama wa mwanamuziki wa kike mashuhuri nchini Tanzania, Zuchu alisifia binti yake akisema amemlea kwa mila na desturi za kukaa kwenye ndoa hivyo hana shaka na maumuzi ya Mwanawe atakayofanya ifikiapo tarehe 14 mwezi huu.