•Baada ya kutangaza kuachana na Mylee Staicey, Weezdom ametambulisha rasmi mpenzi wake mpya kwenye mitandao yake ya kijamii.
•Hii imewadia siku chache baada ya Weezdom kuonya aliyekuwa mpenzi wake, Mylee kukoma kutumia jina lake kwenye mahojiano na wanahabari
Baada ya kutangaza kuachana na Mylee Staicey, Weezdom ametambulisha rasmi mpenzi wake mpya kwenye mitandao yake ya kijamii.
Hii imewadia siku chache baada ya Weezdom kuonya aliyekuwa mpenzi wake, Mylee kukoma kutumia jina lake kwenye mahojiano na wanahabari.
“Mwambieni Mylee Staicey kuwa Mungu alinipa uwezo wa kumjua. Na mimi niko na ushahidi wa kila kitu kuhusu mahusiano yangu na yeye , hivyo aache kutumia jina langu kutengeza kiki, sitaki tuaibishane,” alisema Weezdom
Wiki hii, amepakia picha kwenye ukurusa wa instagram, picha ambayo ilikuwa inaonyesha wapenzi hao wawili.
Mashabiki wametumia sehemu ya maoni kumtania kwa kasi aliyoingia kwenye mahusiano mengine.
@scolasticakivina-haraka ajee
@muthoni__mugo- Unasonga kuliko boda mtu wangu@ djeuphorique-Sawa kaka mimi nimejitoa kuwa wewe ni ndugu yangu kabisaaaa