Mimba sio ugonjwa,'Wanamitandao wamwambia Nandy huku akiwasuta

Muhtasari
  • Kurasa kadhaa za udaku zilimfikia mwimbaji huyo kwa ujumbe wa pongezi, jambo ambalo lilimlazimu kujibu
Msanii wa bongo fleva Nandy
Msanii wa bongo fleva Nandy
Image: INSTAGRAM

Mwimbaji wa Tanzania, Faustina Charles Mfinanga anayejulikana sana kwa jina  Nandy amezidisha ripoti za ujauzito kwa mara nyingine tena baada ya kutoka na vazi lililowaacha baadhi ya mashabiki wake na maswali.

Kurasa kadhaa za udaku zilimfikia mwimbaji huyo kwa ujumbe wa pongezi, jambo ambalo lilimlazimu kujibu.

Katika moja ya jumbe hizo, Nandy alijibu kwa kejeli maswali ya iwapo ni mjamzito au la kwa njia ya kitambo sana bila kukanusha au kukubaliana.

“Umegundua nini kwa hii picha,"Mmoja wa mashabiki wake aliuliza..

Kwa haraka msanii Nandy alijibu ujumbe wa shabiki huo na kusema ;

“Kwamba uyo dada ana mimba anaifichaaaa yaaani hata sijui kwann anafanya ivyooo khaaaa 😮."

Shabiki mwingine alifika kwa mwimbaji huyo akimwambia kuwa Mimba sio ugonjwa "Nandy Mimba sio ugonjwa"

Naye akajibu "kwani nimesemaaa naumwa 😢,".

Hii si mara ya kwanza kwa Nandy kulazimishwa kushughulikia tetesi za ujauzito. Mnamo Januari, alikanusha tena madai kwamba alikuwa na ujauzito wa mchumba wake Billnass, pamoja na maoni potofu kwamba anaweka habari mbali na macho ya umma.

Mwimbaji huyo aliweka wazi kuwa hakuwa na ujauzito, na kuongeza kuwa atakapopata ujauzito habari hizo hazitafichwa kwa mashabiki wake.