Chanzo cha utajiri wa mumewe Vera Sidika chafichuliwa

Vera alisema mumewe ni mwenye bidii ambaye anapenda tu kuweka biashara yake chini ya maji.

Muhtasari

•Kulingana na uchunguzi wa kina wa Google, ilibainika kuwa ana duka la mavazi linaloitwa Mauzo Collections.

• Na inaonekana, anamiliki lebo yake ya muziki ambayo aliondoka Ogopa Dj's kwenda kuanzisha.

Image: INSTAGRAM// VERA SIDIKA

Baada ya Vera Sidika kugombana na mwanasosholaiti mwenzake Amber Ray, udadisi wa watu kuhusu kazi ambayo mume wa Vera anafanya ili kujipatia riziki ulipanda hadi viwango vya juu sana.

Katika ugomvi wao mkali mtandaoni, Amber alisema Brown Mauzo hana kazi na kumwambia kwamba alikuwa na nafasi ya kazi kwake.

Huku akimjibu Vera, Amber aliendelea kumshambulia akisema kuwa yuko tayari kumtafuta mume wake Brown Mauzo ili atumbuize kwenye baby shower yake.

"Unadai kututia moyo lakini huwezi kufanya mtu wako apate kazi.

Hata hivyo, napananga baby shower na niko tayari kumlipa ili atumbuize angalau tuone kama talanta itakubali apate kakitu." Amber aliandika kwa hasira.

Hii iliwafanya watu kufikiria sana, huwa hatuoni Mauzo akifanya matamasha au kualikwa kutumbuiza kwenye hafla hata vilabu. Ndio, huwa anatoa wimbo kila baada ya muda fulani kutukumbusha kuwa yeye ni mwimbaji lakini hiyo pekee ndiyo amewahi kufanya.

Hata hatangazi muziki wake kama wenzake wa Kenya na Afrika Mashariki. Kwa hivyo, malipo ya YouTube kwa nyimbo zake chache ambazo hazijavuma sana hayawezi kuwa jinsi anavyoendeleza maisha yake, maisha ya mke wake na watoto wao pia.

Kwa hivyo Brown Mauzo anafanya kazi gani?

Ana chaneli ya YouTube ambayo ina watu waliojisajili, elfu 84.1, hata hivyo, cha kufurahisha vya kutosha, haina video zake za muziki.

Kila kitu kinaonekana kufutwa na chapisho pekee lililobaki ni la miaka 2 iliyopita wakati Vera alimsurprise kwa siku yake ya kuzaliwa.

Kulingana na uchunguzi wa kina wa Google, ilibainika kuwa ana duka la mavazi linaloitwa Mauzo Collections.

Lina matawi machache Mombasa, alidokeza mipango ya kufungua moja Nairobi pia lakini hiyo haikuzaa matunda. Na inaonekana, anamiliki lebo yake ya muziki ambayo aliondoka Ogopa Dj's kwenda kuanzisha.

Jina la lebo yake ni fumbo ingawa baadhi ya tovuti zinapendekeza kuwa inaitwa Mauzo Classic na inaonekana wakati fulani alimsaini Akothee kabla ya umaarufu wake kuvuma na kuondoka.

Akimtetea mumewe dhidi ya kuchunguzwa na umma Vera alisema kuwa yeye ni mtu mwenye bidii ambaye anapenda tu kuweka biashara yake chini ya maji. Inaonekana ya kutiliwa shaka kwa sababu bila kutangaza unapataje wateja na wawekezaji?

Lakini anaweza kuwa sahihi, mabiashara tajiri kulingana na soko lao lengwa na wateja hawazunguki kujitangaza.

Vera kwa nyakati tofauti amekanusha vikali kuwa yeye ndiye anayefadhili mtindo wa maisha wa mume wake lakini wakati huo huo akasisitiza kwamba hakungekuwa na shida ikiwa ndivyo ilivyokuwa.

Anabainisha kuwa, kama mwanamke huru maisha yako lazima yaendelee ikiwa mifuko ya mwanamume wako imejaa au la.