Hongera! Mchekeshaji Awinja afunga ndoa na mwenzake Osoro

Wawili hao walipeleka uhusiano wao katika hatua nyingine siku ya Jumamosi.

Muhtasari

โ€ข Wakati wa hafla hiyo ya Jumamosi, Awinja na Osoro walikuwa wamevalia vitenge vilivyofanana.

โ€ขKwa muda mrefu, Awinja na Osoro wamekuwa wakicheza mume na mke katika michezo yao mingi ya kuigiza

Image: HISANI

Muigizaji mashuhuri wa Kenya Jacky Vike almaarufu Awinja Nyamwalo hayuko sokoni tena kufuatia harusi yake ya kitamaduni na mchekeshaji mwenzake Osoro.

Wawili hao walipeleka uhusiano wao katika hatua nyingine siku ya Jumamosi katika hafla ambayo ilipambwa na marafiki na wanafamilia wao wa karibu. Wakati wa hafla hiyo, Awinja na Osoro walikuwa wamevalia vitenge vilivyofanana.

Video zilizochukuliwa wakati wa hafla hiyo zilichapishwa kwenye mitandao ya kijamii, na kuibua hisia mseto kutoka kwa mashabiki na wafuasi wao.

Hata hivyo, baadhi ya mashabiki walipuuza madai ya harusi hiyo, wengi wakisema kwamba huo ni mchezo mwingine wa ucheshi.

Kutokuwepo kwa marafiki mashuhuri wa Awinja kwenye sherehe hiyo ya kitamaduni kulizungumza mengi. Hii ilifanya iwe vigumu kwa mashabiki kuamini kwamba kweli Osoro na Awinja walikuwa wamefunga ndoa.

Kwa muda mrefu zaidi, Awinja na Osoro wamekuwa wakicheza mume na mke katika michezo yao mingi ya kuigiza - na kufanya iwe vigumu kwa mashabiki kuamini kuwa wao ni wapenzi.

Kufikia sasa video na picha zilizochukuliwa kwenye sherehe hiyo hazijachapishwa na watu wengine pekee - jambo ambalo limezua taharuki kwa mashabiki wanaohoji uhalali wa harusi hiyo ya kitamaduni.

Je, unaamini kwamba Awinja hayuko Sokoni? Muda pekee ndio utasema.

Hizi baadhi ya hisia za Wakenya:-

faithvoline Mko sure si jokes Za awinja za kila siku???

its.muthonii_ Mbona inakaa jokes๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚

sta.muka Amber reeee, Akotheee, Kameneee, Sasa tena huyu... Soko mmesena mtaacha prity vishindo peke yake๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚

jacintamumo19 Napenda venye ametupea suspense hapa๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚hakuna mtu ako sure ni real ama ni comedy๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚ tuwaache tu.๐Ÿ™Œ

jacintamumo19  Napenda venye ametupea suspense hapa๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚hakuna mtu ako sure ni real ama ni comedy๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚ tuwaache tu.๐Ÿ™Œ

iammariah9 Kumbe ilikua serious ivi ๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚ and here I thought ilikua tu content ๐Ÿ˜ฎ๐Ÿ˜ฎ๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚ aki shosho media wewe...love is a beautiful thing ๐Ÿ˜๐Ÿ˜๐Ÿ˜ congrats to them

pascarlian Mko sure si comedy Bora nisione advertisement ya kitenge๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚ anyway congratulations

mtunecessary Kutoka soko ndio ngumu kurudi requires only one text from that bitter ex and voila we are back to wearing boots while walking in the market

vanessa_maurine How are we supposed to believe this?๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚

naomi.misoi Huyu Awinja anapenda jokes sana so hatujui kama hii iko serious or acting. Anyway congratulations if it's true

tessthebossbabe I though all along they were just creating contentโ€ฆnothing serious.Congratulations!๐Ÿฅณ