Hisia mseto baada ya wakaazi wa Juja kung'ang'ania mikate na juisi kufuatia ajali iliyohusisha lori mbili

Baadhi ya wakazi walionekana wakitazama huku wengine wakikimbia na mikate na juisi nyingi kadri ya uwezo wa mikono yao.

Muhtasari

•Wakazi walikimbia kuchukua mgao wao wa bidhaa za bure  baada ya lori mbili zilizokuwa zimebeba vyakula kugongana kwenye barabara kuu ya Thika.

•Baadhi ya Wakenya wamewakosoa waliojisaidia kwa bidhaa hizo za bure, wengine wakitamani wangekuwepo na wengine hata kushangaa jinsi tukio hilo lilivyotokea.

waling'ang'ania mikate na juisi baada ya lori mbili kugongana Jumatatu.
Wakazi wa Juja waling'ang'ania mikate na juisi baada ya lori mbili kugongana Jumatatu.
Image: HISANI

Wanamitandao wa Kenya wameendelea kutoa maoni mseto baada ya wakaazi wa mji wa Juja kung’ang’ania mikate na juisi kufuatia ajali iliyohusisha lori mbili Jumatatu mchana.

Video za tukio ambazo zimesambazwa kwenye mitandao ya kijamii zinaonyesha drama kubwa katika mji huo wenye shughuli nyingi katika kaunti ya Kiambu huku wakazi wakikimbia kuchukua mgao wao wa bidhaa hizo za bure  baada ya lori mbili zilizokuwa zimebeba vyakula kugongana kwenye barabara kuu ya Thika Superhighway.

Ajali hiyo iliyotokea katikati mwa mji wa Juja ilisababisha kumwagika kwa mikate na vinywji vya aina mbalimbali barabarani, na kuvutia umati mkubwa wa watazamaji na wapita njia, kila mtu akitafuta kutoka na kitu.

Katika video hizo, baadhi ya wakazi wanaonekana wakitazama huku wengine wakikimbia na mikate mingi na juisi kadri ya uwezo wa mikono yao.

Maafisa wa polisi walijaribu kuzuia hali hiyo lakini  kufikia wakati mambo yalipoa, vyakula vingi vilikuwa vimechukuliwa.

Wakenya wameendelea kutoa maoni yao kuhusu hali hiyo, wengine wakiwakosoa watu waliojisaidia kwa bidhaa hizo za bure, wengine wakitamani wangekuwepo na wengine hata kushangaa jinsi tukio hilo lilivyotokea.

Tazama maoni ya baadhi ya Wakenya kwenye mitandao ya kijamii;

Lord Abraham Mutai: What are the odds for such an accident 🤔. These are Juja residents scrambling for bread and juice after an accident involving a lorry carrying bread and another carrying  juice along Thika Road. And, must we always loot from accidents scenes?

Vu.vah: Leo macomrades atleast wataonja Ribena.

King.mungai: Waaah, evebody’s childhood dream.

Tv.mounting_: Yes, shame on them. Rather than helping, they take. Mankind.

Kylkihia: And we complain when politicians steal from us.

Kiokod37: Those saying shame on you, hiyo stock hakuna mahali itauzwa ata ikiwa rescued na insurance so wananchi wafurahie.

Kangui_benson: Kila mtu anajua shida zake, stop judging.