Muhtasari
• Msanii na mtangazaji tokea taifa la Tanzania, Babalevo amesema kwamba lazima awe mshindi katika tuzo zilizozinduliwa na BASATA majuzi, tuzo ambazo zitawashuhudia wasanii wakituzwa katika vitengo tofauti.
• Aidha, akichapisha ujumbe katika ukurasa wake wa Instagram, Babalevo ameonya kwamba mara hii hawataki upendeleo katika utoaji wa tuzo hizo na kwamba kila msanii awe na mazingira sawa ya kuwania bila kushurutishwa kwa namna yoyote ile.
• ‘Dokta’ kama anavyotambulika kwa sasa pale Bongo, msanii huyo anazidi kufanya vizuri huku akitia kibindoni hela nyingi kupitia mikataba ya ubalozi kwa kampuni mbalimbali.