Asamoah Gyan kumpa Ex wake nyumba UK na Accra, kituo cha kuuza petroli na magari 2

Kando na hayo, mchezaji huyo wa zamani pialazima pia alipe cedis 25,000 za Ghana (Shilingi za Kenya 317,520) kwa mwezi kwa ajili ya malezi ya watoto.

Muhtasari

• Kabla ya kufunga ndoa rasmi miaka 10 iliyopita, wenzi hao walikuwa na watoto wawili.

• Gyan alitangaza kustaafu soka mwezi Juni, akiwa amefunga rekodi ya taifa ya mabao 51 katika michezo 109 aliyoichezea nchi yake.

Asamoah Gyan
Asamoah Gyan
Image: X

Mahakama nchini Ghana imemuamuru mchezaji wa zamani wa soka Asamoah Gyan kumpa mkewe wa zamani mgao wa mali zake nyingi kama fidia baada ya kubainishwa kwamba yeye ndiye baba wa watoto wa mwanamke huyo watatu, BBC Sport wamebaini.

Kijana huyo mwenye umri wa miaka 37 alitakiwa kumpa Gifty Gyan nyumba nchini Uingereza, nyumba mjini Accra, kituo cha kuuza mafuta na magari mawili.

Gyan na mke wake wa zamani wamekuwa kwenye vita vya kisheria kwa miaka mitatu, huku kesi ya talaka ya wanandoa hao ikitolewa kufuatia madai ya mwanasoka huyo kutokuwa mwaminifu dhidi ya Gifty Gyan na madai yake kwamba watoto wao watatu huenda wasiwe wake.

Uchunguzi wa DNA ulikanusha madai yake kwamba hakuwa baba mzazi wa watoto hao.

Siku ya Jumanne, mahakama iliamua kwamba fowadi huyo wa zamani wa Udinese, Rennes na Sunderland lazima pia alipe cedis 25,000 za Ghana (Shilingi za Kenya 317,520) kwa mwezi kwa ajili ya malezi ya watoto.

Ingawa wenzi hao walikuwa tayari wametengana, mahakama ilibatilisha ndoa hiyo kufuatia ombi lililojazwa na Asamoah Gyan.

Mahakama iliamua kwamba Gifty Gyan alikuwa ametoa mchango usio wa pesa katika ununuzi wa mali hizo kwa sababu ni yeye pekee aliyekuwa akiwalea watoto wao huku Gyan akifanya biashara yake.

Nyumba ya vyumba vinne huko Accra ilinunuliwa kwa ajili yake kabla ya ndoa yao ya 2013. Kabla ya kufunga ndoa rasmi miaka 10 iliyopita, wenzi hao walikuwa na watoto wawili.

Gyan alitangaza kustaafu soka mwezi Juni, akiwa amefunga rekodi ya taifa ya mabao 51 katika michezo 109 aliyoichezea nchi yake.

Pia ndiye mfungaji bora wa Afrika katika Kombe la Dunia - akiwa na mabao sita katika matoleo ya 2006, 2010 na 2014 - na alicheza katika mashindano saba ya Kombe la Mataifa ya Afrika, na kusaidia Black Stars kumaliza nafasi ya tatu 2008 na kama washindi wa pili 2010 na 2015. .

 

BBC iliwasiliana na mchezaji huyo wa zamani wa kimataifa wa Ghana kwa maoni yake kupitia usimamizi wake, lakini alikataa.