“Wanangu ni kama mimi, Siwafundishi ila wanaona na kujifunza bidii kupitia mimi” – CR7

'Kweli, watoto wangu, ni kama mimi. Siwafundishi ila wanaona kwa mfano kwani wakati mwingine nikishindwa nakasirika, wakati mwingine nalia, inategemea na wakati.’

Muhtasari

• 'Wanafanana, hivyo hata na watoto wangu ninashindana, huwa nataka kushinda. Sitoi chochote bure.'

• Ronaldo ana watoto wawili na mpenzi wake Georgia Rodriguez, huku akiwazaa wengine watatu na mwanamitindo huyo wa Argentina-Kihispania, ambao wote walizaliwa kupitia surrogate.

RNALDO NA FAMILIA YAKE
RNALDO NA FAMILIA YAKE
Image: hisani

Cristiano Ronaldo amefunguka kuhusu maisha ya familia yake nje ya soka na jinsi makali yake ya ushindani yamepitishwa kwa watoto wake.

Gwiji huyo wa Ureno anajulikana sana kwa hamasa yake ya kuvunja rekodi ndani ya soka, hata akiwa na umri wa miaka 39.

Wiki iliyopita tu, Ronaldo amekuwa mchezaji wa kwanza katika historia ya soka kufunga mabao 900 katika maisha yake ya soka alipoifungia Ureno dhidi ya Croatia.

Na alipozungumza na mchezaji mwenzake wa zamani wa Manchester United, Rio Ferdinand, mfungaji huyo wa mabao alifichua kwamba ushindani wake umeenea hadi kwenye shughuli na watoto wake watano.

'Nilikuwa kwenye Bahari Nyekundu siku chache zilizopita, nacheza kila siku padel. Mimi na Cristiano Jr tunakasirika, hatuongei kwa siku mbili,' aliambia podikasti ya Rio Ferdinand Presents.

'Hii ndiyo sababu nina furaha, hata yule mdogo Matteo [anapata ushindani], napenda. Inaonyesha wana utu.

'Kweli, watoto wangu, ni kama mimi. Siwafundishi ila wanaona kwa mfano kwani wakati mwingine nikishindwa nakasirika, wakati mwingine nalia, inategemea na wakati.’

'Wanafanana, hivyo hata na watoto wangu ninashindana, huwa nataka kushinda. Sitoi chochote bure.'

Ronaldo ana watoto wawili na mpenzi wake Georgia Rodriguez, huku akiwazaa wengine watatu na mwanamitindo huyo wa Argentina-Kihispania, ambao wote walizaliwa kupitia surrogate.

Manawe mkubwa, Cristiano Jr, anajaribu kufuata nyayo za fowadi huyo mashuhuri na kwa sasa anachezea kikosi cha vijana cha Al-Nassr cha Saudi Arabia, huku Ronaldo akiendelea na ubia wake na timu ya wakubwa.

Cristiano Jr, ambaye ana umri wa miaka 14, amemfuata babake popote alipocheza, akishirikiana na akademi za Juventus na Manchester United.

Lakini licha ya maendeleo ya mwanawe katika mchezo huo, Ronaldo ana nia ya kutodai mengi kutoka kwa kijana huyo mwenye kipaji.

"Kizazi hiki, ni vigumu kuwaambia kitu na kuwaacha wafanye," aliendelea. 'Siku zote watamwona baba yao kama mfano, wananiona kila siku katika kile ninachofanya, nyumbani, mazoezini au katika mchezo. Wananiona nafanya kazi sana.