Simba alimua kuweka video mtandaoni akionyesha eneo lake la kuegesha magari likiwa na magari yote pamoja na lililokuwa likimilikiwa na Donna .
Hatua yake imejiri siku chache tu baada ya Mbosso kukanusha ripoti kwamba alikuwa amekabidhiwa gari la Tanasha
Mbosso alisema, tayari bosi wake Diamond alikuwa amemueleza kwamba kutakuwa na sakata kuhusu gari lake kufanana na la Tanasha
&feature=emb_logo
“Hata wakati nanunua hili Gari hata Diamond mwenyewe aliniambia usipochunga mdogo wangu Gari lako litaonekana la Tanasha. Lakini nafikiria pia tunaweza kulipeleka hili gari mpaka kwa Diamod kule alafu tupige picha zikiwa zote, ile ya Mama Dangote, Tanasha na hii Hapa. Chombo changu na Nashukuru Mwenyezi Mungu ndo nimekianzia mwaka nacho, ndo linafikisha kama Mwezi hivi,” Amesema Mbosso.
Mbosso Khan pia alitoa log book ya gari lake ili kuthibitisha kwamba halikuwa lake. Katika mahojiano hivi maajuzi, Donna amesema halihitaji gari ambalo alipewa na Diamond kwa sababu ana lake la BMW Nairobi