Mvulana mwenye umri wa miaka mitano Ethan Macharia amemwandikia barua rais Uhuru Kenyatta baada ya yeye na mamake kukwama nchini India kwa wiki kadhaa wlaiposhindwa kulipia gharama ya upasuaji anoafaa kufanyiwa.
Katika barua hiyo yenye kitangulizi "Dear Mr President," Ethan amemraia rais Kenyatta na wahisani wengine kumsaindia kuchangisha shilingi milioni 3.5 ili kufanikisha upasuaji anaofaa kufanyiwa . Mtoto huyo alianguka mwezi Novemba mwaka wa 2018 na kuumia kichwa walipokuwa akicheza .Baadaye hali yake ilizoroteka na kuanza kupatwa na hali mbaya zinazomsababishia madhara ya kimwili anapojipata bila fahamu .
Mamake Ethan ,Veronica Njeri, amesema maisha yao yalikuwa ya kawaida hadi siku hiyo ya mkasa na wamekuwa nchini India kwa miezi 14 wakijaribu kupata pesa za kumwezesha mwanawe kupata matibabu anayohitaji kuboresha hali yake . Ethan hajaweza kurejea shuleni tangia hapo na anasema anataka kuwa mchezaji wa soka akiwa mtu mzima .