Ghost Mulee aitetea Harambee Stars, ataja sababu za kupoteza

Wanyama-Victor-vs-Mozambique
Wanyama-Victor-vs-Mozambique
Ghost Mulee ametaja sababu za timu ya kitaifa ya Harambee Stars kupoteza moja kwa nunge.

Katika kipindi kinachoruka katika kituo hiki kila asubuhi cha Patanisho, Ghost amesema kuwa uwanja kuteleza ulichangia timu ya kitaifa kupoteza.

Kuteleza kwa uwanja kulisababishwa na mvua mkubwa iliyonyesha kabla mechi kuanza

Harambee Stars walikabana koo na timu ya soka ya Msumbiji katika mechi ya kirafiki Alasiri jana.

Hii ilikuwa jaribio kubwa la kutia makali kwa michuano ya kufuzu kwa AFCON mwaka wa 2021

Kabla mechi hiyo kuanza, Francis Kimanzi alikuwa na matumaini makubwa zaidi huku akisema wachezaji hao ambao wamekuwa kambini kwa siku tano katika mazoezi ya kina.

Ghost amesema kuwa timu ya kitaifa haifai kupoteza matumaini yoyote.