Wetangula na Wamalwa wazika tofauti zao na kuapa kushirikiana

Wazee wa baraza la jamii ya wabukusu hii leo wamewafanikiwa kuwapatanisha seneta wa kaunti ya Bungoma ambye pia ni kinara wa chama cha Ford Kenya Moses Wetangula na waziri wa ugatuzi Eugene Wamalwa ili jamii ya wabukusu iweze kuwa na umoja.

Mwenyekiti wa baraza hilo Richard Walukano amesema kwamba muungano wa jamii hio ambayo ndio yenye idadi kubwa kwa jamii za mulembe utawezesha jamii zingine za eneo hilo kuungana na kuhesimiwa na jamii zingine kisiasa.

Wetangula na Wamalwa walikubali kuzika tofauti zao za muda wa miaka tisa wakisema kwamba todfauti zao za kisiasa zimesababisha wakaazi wa Bungoma na Transzoia kubaki nyuma kimaendeleo.

Brian O. Ojamaa