PATANISHO: Marafiki yangu walinishawishi nitoe mimba ya bwanangu

gidi na ghost
gidi na ghost
Mara nyingi Gidi hupokea SMS za kuomba msamaha kutoka wanaume  ambao wangependa  kupatanishwa na wake zao.

Yule ambaye angependa kupatanishwa hivi leo ni Juliet ambaye alikosana na bwanake Joseph 2017.

Mwanadada huyu alimwelezea Gidi kwamba waliachana 'tukielekea election 2017'.

Tulikosana tuu kidogo nilikuwa na mimba yake, tukakosana maneno ya nyumba, akanirushia vitu zangu inje, na alafu nikatoa mimba yake.

Katika hiyo harakati nikatoka nikaenda kuka kivyangu, tukaachana kwa muda ya mwezi mmoja. lakini nikaona turudiane, na vile tuu tulirudiana nayeye akaamua kutoka. Venye alijua tuu alinipa mimba ingine, nayeye akabeba vitu akahama.

Mume wake alienda wapi?

Ata sijui penye alienda. mimi nilikuwa nimeenda job kurudi watu wanniambia na si mulihama, ati alijuja akabebea vitu zake. Ata sikujua niko na mimba.

Je, bwanake aligundua aje bibi ana mimba na hakuambiwa?

Ata sikuwa najua mwenyewe nina mimba Lakini mi si najuanga mwanamume akinipea mimba sasa mimi..he..(akicheka)

Nilichanganikiwa. 

Ata nilijifungua, mtoto ni mkubwa ako na nine months, hajashugulika kujua huyu mtoto ako aje alimwaona tuu mara moja, Mara ya mwisho kuongea na yeye ilikuwa last month,ata kama ameoa nataka turudiane.'

Je msimamo wa bwana Joseph ni yapi?

'Mimi nilimsamehe kitambo, na nimeshaa oa na atafute bwana ikiwa yeye anataka kuoa. ikiwa ni mambo ya mtoto asijali sana hiyo ni kitu kidogo.

Skiza kanda usikie mawaidha ya Gidi kwa Juliet ikiwa bwana amekataa kushugulikia mtoto kuna mwongozo wa sheria ikiwa mume amekataa kumshurutisha.