Swali hili la wanahabari lilitokea katika mstari kwa wimbo wa Uno unaomtaja Mondi na Zari.
Kikundi cha wanahabari nchini kiliachwa kwa mshangao mkubwa na kudai kuwa Harmonize alionyesha dharau kubwa kwao.
Harmonize ambaye amepanga msururu wa safari katika nchi mbalimbali kuipa nguvu ngoma hii alisubiriwa na wanahabari hao kwa masaa mengi.
Jeshi alitakiwa kuhutubia kikao hiki cha wanahabari kabla kuendelea na safari yake.
Katika ziara hii, Harmonize C.E.O wa Konde Gang anapania kuipeleka nyimbo ya Uno hadi iwafikie watu wa tabaka mbalimbali.
Harmonize alianza safari hii na gang yake nchini Tanzania.
https://www.instagram.com/p/B4KjCqOlLUp/
Alimwaga mtama wote A-Z kuhusu lebo ya WCB na baadae akafanya party kubwa ya wanahabari huku akiperform Uno.
Kikao chake na wanahabari Kenya kilisubiriwa saa tano mchano na baadae akasukuma hadi saa tisa alasiri.
Kikao hicho baadae kilisongezwa hadi saa moja jioni. Hii ina maana kuwa wanahabari hao walimsubiri siku nzima.
Je, unadhani ni kitu gani kilimfanya Mmakonde huyu kuwazimia data wanahabari Kenya?
Kama desturi za vikao hivi, wanahabari walikuwa washatua eneo la Blue Door VIP lounge kumsubiri staa huyu.
Kwa tendo la kejeli zaidi, walinzi wa staa huyu walisukuma viti na kumpisha atoke kwenye kikao.