Gavana wa Nairobi Mike Sonko amelifanyia mabadailiko baraza lake la mawaziri .Kupitia arifa iliyotolewa ijumaa ,Sonko Amemrejesha afisini Charles Kerich kama waziri wa ardhi na mohammed Dgane amerejeshwa katika idara ya barabara . Pauline Kahiga aliyekuwa akihudumu kama waziri wa Ardhi na Fedha amefurushwa .
Larry wambua ambaye alikuwa akihudumu katika idara ya ugatuzi sasa amehamishwa hadi katika ile ya mazngira .Vesca Kangogo ambaye amekuwa akihudumu kama waziri wa mazngira na kaimu waziri wa afya amehamishwa hadi katika wizara ya ugatuzi .
Hitan Majevda sasa ndiye waziri wa kaunti wa afya ilhali Newton Munene na Lucia Mulwa wamesalia katika nafasi zao za ICT na elimu mtawalia .Winfren Gathangu pia ameonyeshwa mlango baada ya kufutwa kazi kama waziri wa kilimo .Sonko amewateua George Osewe (Biashara ) na Karen Nyamu kujiunga na baraza lake la mawaziri . Mwaka jana Sonko aliwasimamisha kazi maafisa 16 wakuu wa kaunti baada ya mkasa wa kuanguka kwa shule ya Precious Talent Academy na kusababisha vifo vya wanafunzi wanane .