'Wasafi wote inaonekana mnapenda ngono,’ Queen Darleen awakashifu wasanii wa WCB

28766466_206620433426578_6680409410851831808_n-696x696
28766466_206620433426578_6680409410851831808_n-696x696
Queen Darleen dada yake staa wa bongo Diamond Platnumz ametoa wimbo wake mpya unaofahamika kama ‘bachela’ wimbo ambao amemshirikisha msanii wa lebo ya WCB Lava lava.

Katika kibao hicho Lava Lava azungumzia jinsi alivyo mchanga na anataka kufurahia maisha bali hataki kujihusisha na uhusiano wa kimapenzi

Kwa upande mwingine anazungumzia vile kuwa katika ndoa ni jambo muhimu na lenye furaha.

Mwaka jana Queen aliolewa kuwa mke wa pili wa mchumba wake katika harusi ya siri.

“Nina ng’aa mume wangu ametumiliki sisi wawili.” Wimbo wake uliimba.

Naye lavalava alijibu,

“Katika mtandao wa kijamii wa instagram wakosolewa hukuambiwa kuwa ulinyakua mume wa wenyewe

Kwa sababu ya pesa na ukakubali kuwa mke wa pili, ni afadhali niwe Bachela.”Alijibu Lavalava.

Katika wimbo huu, Lavalava alinakili na kusema hataki kile kilimfanyikia msanii Diamond na Tansha kimfanyikie.

“Uliza Dangote, alizushana na Tanasha na akaacha kutufollow sisi sote.”

Naye Queen Darleen aliendelea na kutema yote chini.

“Wasafi wote, inaonekana mnapenda ngono.” Alisema Queen.

Baada ya ndugu yake kuachana na Tanasha, amekuwa akiwaambia mashabiki kuwa Diamond ni bachela.

Huku maji yakizidi unga na kumshawishi aliyekuwa mpenzi wake Wema Sepetu aweze kumrudia Diamond.

Hiki hapa kibao cha bachela;