Mwanamuziki wa nyimbo za kikuyu Samido amekuwa na mengi ya kusimulia kuhusu safari yake katika sanaa , Mwanamuziki huyo pia ni afisa wa polisi na hilo halijamkosesha fursa ya kuendeleza talanta yake katika muziki .
Samido akizungumza na Massawe Jappani amesimulia jinsi alivyoteseka utotoni na majirani walimsaidia kusoma kwa kumlipia karo . Alianza kuimba mwaka wa 2009 akimsaidia mwanamuziki Kamande wa Kioi
Kuhusu kali yake ya polisi anasema ;
"Kitengo cha polisi ni kama tumbo la mama. Tumbo la mama linaweza kuzaa, pasta na watu wengine. Watoto wote hawawezi kuwa sawa au kufanana..."
Samido anasema wakati alipopata kazi ya polisi alikuwa hana shati na hawezi kuiacha .
"Kazi ya polisi niliitafuta bila shati. Nilikuwa ninapitia shida sana na ilikuwa kama kivukio kwangu..."
Ameongeza kusema ;
"Changamoto kubwa katika maisha yangu kwenye familia, muziki, na kazi yangu kama afisa wa polisi ni muda..."