Mfanyibiashara Chris Obure amelazwa hospitalini baada ya kusema kwamba ni mgonjwa .
Hilo linafika kabla ya kufikishwa kwake kortini leo ambapo mahakama inafaa kutoa uamuzi kuhusu ombi lake la kutaka kuachiliwa kwa dhamana .
Upande wa mashtaka unapinga kuachiliwa kwake kwa dhamana ukidai kwamba hatua hiyo itavuruga uchunguzi dhidi yake .
Obure pamoja na mlinzi wake Robert Bodo wanakabiliwa na mashtaka ya kumuua Kevon Omwenga .Siku ya alhamisi walishtakiwa pia kwa kutoiweka ifaavyo bunduki . Bunduki hiyo ndio iliyotumika katika mauaji ya Omwenga