Mbivu na Mbichi:Omboko Milemba, Rozah Buyu waongoza katika orodha ya wabunge bora

Milemba
Milemba
Mbunge wa Emuhaya Omboko Milemba  ameorodheshw akama mbunge bora kwa utendakazi .

Utafiti  uliofanywa na  Infortrak na kutolewa siku ya jumapili umeonyesha kwamba Milemba  alishikilia nafasi ya kwanza kwa asilimia 75.4

Utafiti huo ulilenga kujua jinsi watu wa  maeneo bunge walivyowaorodhesha wabunge  wao ,maseneta  ,waakilishi wa akina mama,MCA na magavana  kati ya novemba/disemba  mwaka jana hadi januari mwaka wa 2020.

Utafiti wa mwanzo ulifanywa kati ya agosti na septemba mwaka  wa 2019

Jumla ya watu elfu 37,600 walihojiwa katika kaunti zote 47 .

Kulingana na utafiti huo Milemba anafutwa na , mbunge wa  Emurua Dikiri Johana Ngeno katika nafasi ya pili kisha mbunge wa Mwala  Vincent Musyoka ni wa tatu kwa asilimia 70.8

Wengine ni Christopher Aseka wa Khwisero kwa nafasi ya nne akiwa na asilimia 70 na Patrick Musimba wa Kibwezi West aliye na asilimia 69.8

Kulingana na utafiti huo mbunge wa  , Isiolo South  Abdi Koroputepo ndiye mwenye utendakazi duni Zaidi akiwa na asilimia 33.0

Mwingine katika nafasi ya pili kutoka chini  ni Clement  Muturi wa Kangema  akifuatwa na  Francis Kuria wa Molo

Mbunge wa Taveta Naomi Shaban anaongoza orodha ya  wabunge bora wa kike  akiwa na asilimia 61.6

Anafutwa na mbunge wa Kitui West MP Edith Nyenze akiwa na  asilimia  58.4 mbunge wa Samburu West P Naisula Lesuuda akiwa na asilimia  57.5 ,Mary Njoroge wa maragwa akiwa na asilimia  56.8  na mbunge wa  Malindi  Aisha Jumwa akiwa na asilimia 53.3

Wakati huo huo mwakilishi wa akina mama wa KISUMU Rozah Buyu anaongoza orodha ya waakilishi wa akina mama wanaofanya vyema akiwa na asilimia 61.5

Anafuatwa na mwenzake nwa Homa bay Gladys Wanga  kisha  mwenzao wa  Lamu Ruweida Mohamed ni wa tatu

Mwakilishi wa akina mama wa  Kiambu' Gathoni Wamuchomba ndiye aliye na utendakazi duni sana akiwa na asilimia 39

Mwingine ni Janet Nangabo wa Trans Nzoia akifutwa na mwakilishi wa Nyamira Jerusha Mongina

Mbunge wa Kapseret   Oscar Sudi,  ambaye ni mtetezi mkubwa  wa naibu wa rais William Ruto  mbunge wa makadara George Aladwa na mbunge wa  Nakuru Town west  Samuel Arama ni miongoni mwa  wajumbe ambao hawakusema lolote bungeni mwaka wa 2019

Wengine ambao hawakutamka lolote bungeni ni mbunge wa   Shinyalu Justus Kizito, Alfred Sambu wa  Webuye East na John Naicca wa Mumias West.