Jamaa wa ‘Covid millionaires’ miongoni mwa watu 3 waliokamatwa wakijifanya kuwa maafisa wa EACC na KRA wakiitisha hongo ya milioni 2

gORDON
gORDON
Jamaa aliyehojiwa akifichua sakata ya wizi wa fedha katika kemnsa kupitia Makala ya upekuzi ya  Covid millionaires ' ni miongoni mwa watu watatu waliokamatwa wakijifanya kuwa maafisa wa EACC na KRA na kuitisha hngo ya shilingi milioni 2 .

 Godwins Agut ambaye ni mkurugenzi wa  shirika la  Network Action Against Corruption  alihusishwa katika Makala hiyo ya upekuzi  iliyotayarishwa na NTV  na kusimulia jinsi mabilioni ya kupambana na Covid 19 na misaada iliyotolewa na  bwenyenye Jack Ma ilivyotumiwa vibaya .

Agutu  alikamatwa pamoja na Alex Mutua  na Ken Kimathi siu ya jumatano usiku . Watatu hao wanashtumiwa kwa kumteka nyara mkurugenzi wa  Hi-tech Enterprise  wakijifanya kuwa maafisa wa KRA  na EACC kabla ya kuitisha hongo ya shilingi milioni 2 .

Mkuu wa DCI George Kinoti amesema watatu hao walikuwa wakishirikiana na watu wengine watatu ambao bado hawajakamatwa .

Watatu hao wanadaiwa kuwa wafanyikazi wa KRA waliotajwa kuwa  ;Houdouvia Njoroge, Harrison Ochar na  Brian Kimemia.

Walitumiwa magari mawili ya Prado yenye nambari za usajili  GKB 070B  na  KCY 280Q  na kuvamia afisi za mwathiriwa wao jijini Nairobi septemba tarehe 26  na kuichukua tarakilishi bebe yake .

" washukiwa hao walirejea tena septemba tarehe 29  na kuitisha shilingi milioni 2 kutoka kwa mwathiriwa na alipokosa kuzipata pesa hizo walimuingiza katika gari moja la GKB na kisha kumpeleka katika jumba la  Lutheran Hse  kwenye barabara Nyerere," Kinoti  amesema

Kinoti  ameongeza kwamba walimlazimisha mwathiriwa kuwapigia jamaa zake simu na walifaulu kukusanya shilingi nusu milioni  na washukiwa wakaenda hadi nyumbani kwa mwathiriwa wao mtaani westland kuzichukua pesa hizo .

" Uchunguzi ulianzishwa na washukiwa wattau hao walikamatwa katika  jumba la  Lutheran House,  huku ikigunduliwa kwamba nambari ya usajili  ya gari walilotumia  GKB 070B ni gari Land Rover Discovery  ambalo linatumiwa na idara ya mahakama’  Kinoti amesema