Unyama!Mwanamke atiwa mbaroni kwa madai ya kuwatupa wanawe kwa kisima,1 aaga dunia

Pingu
Image: Radio Jambo

Mwanamke amekamatwa baada ya kuwatumbukiza wanawe wawili ndani ya kisima cha maji Jumatatu asubuhi saa 10 asubuhi, DCI imesema.

Katika tukio lililowashtua wakaazi wa kijiji cha Chepkogen huko Chemaner, kaunti ya Bomet, mama huyo, Sharon Chebet, aliwalazimisha wavulana wake wawili, wa miaka sita na miaka minne, kuingia kwenye kisima cha maji cha mita 40 na kuwaacha wazame.

DCI alisema kuwa kwa bahati nzuri, jirani aliwasikia wavulana hao, wakiwa kwenye kisima hicho.

"Pamoja na watu wengine wenye nia njema, waliungana na kuwaokoa wavulana waliomwagiwa maji, kabla ya kuwakimbiza katika hospitali ya rufaa ya kaunti ya Longisa," DCI alisema.

Mvulana wa miaka sita aliokolewa kutoka ukingoni mwa kifo na wasamaria wema, lakini kaka yake wa miaka minne aliaga dunia.

Mama yao mwenye umri wa miaka 22 alikamatwa mara moja kwa kitendo hicho cha kinyama na sasa yuko chini ya ulinzi akissubiri kushtakiwa.

"Kwa kusikitisha, mvulana huyo wa miaka 4 alipita wakati kaka yake mkubwa alinusurika . Mama yao mwenye umri wa miaka 22 alikamatwa mara moja kwa kitendo hicho cha kinyama na sasa yuko chini ya ulinzi akishughulikiwa kwa kushtakiwa,"Ilisema DCI.