•Mwandani huyo wa naibu Rais William Ruto akizungumza alisema wazi wamechoka na historia ambayo imekuwa ikitajwa kila wakati.
•Mdahalo mkubwa ulizuka katika mtandao wa Twitter baadhi ya Wanamitandao wakimkumbusha Kihika historia yake.
Seneta wa Nakuru Susan kihika amejiipata pabaya kosolewa kufuatia maneno aliyotoa kuhusu kinara wa ODM Raila Odinga.
Mwandani huyo wa naibu Rais William Ruto akizungumza alisema wazi wamechoka na historia ambayo imekuwa ikitajwa kila wakati ilhali hakuna anayesema vile nchi itakuwa katika siku za usoni
“Tumesikia sana kuna wengi wametembea na kila wakati wakipewa kipaza sauti hawatwambii chenye watafanya tukiendelea mbele, wanatwambia mambo ya zamani, wamekwama kwa historia”
Maneno haya hayakuchukuliwa rahisi na baadhi ya wakenya ambao walieleza ghadhabu yao kupitia mitandao ya kijamii.
Mdahalo mkubwa ulizuka katika mtandao wa Twitter baadhi ya Wanamitandao wakimkumbusha Kihika historia yake.
@Airo Nick “wale hawajui historia Baba anawakumbusha”
@Brigade Ole “Kama unasimama lazima tujue historia. Afadhali tuchague shetani tunamjua kuliko malaika hatumjui”
Susan ambaye anamezea kiti cha ugavana kaunti ya Nakuru kiti kinachokaliwa na Lee kinyanjui amekuwa akiendesha kampeni moto katika ngome hiyo inayokisiwa kuwa na waungaji mkono wengi wa mrengo wa UDA.
Kihika hajawasaza wanaomkosoa mitandaoni huku akiwajibu kupitia mtandao wake wa twitter.
Agreed. No FAKE history. Otherwise let Kitendawili tell us how he LED a COUP to Overthrow Moi’s democratically elected Govt in 1982 and even bragged about it in a book. Not edited, self serving history but the REAL History! 🙏🏼 https://t.co/MsVdJpZd8M
— Sen. Susan Kihika (@susankihika) December 16, 2021