Raila Junior amshauri Moses Kuria ajiunge na Azimio baada ya kukutana naye Dubai

Muhtasari
  • Katika ukurasa wake wa twitter, msaidizi huyo alisema alishangazwa na maendeleo ya Kuria ya kupona

Mwanawe kiongozi wa ODM Raila Odinga Raila Junior ndiye Wakenya wa hivi punde zaidi ambao wamemtembelea au kukutana na Mbunge wa Gatundu Kusini Moses Kuria huko Dubai.

Mbunge huyo amekuwa katika hospitali ya Dubai kwa wiki kadhaa kuuguza majeraha ya moto aliyopata kwenye miguu yake.

Katika ukurasa wake wa twitter, msaidizi huyo alisema alishangazwa na maendeleo ya Kuria ya kupona.

Pia alifichua kuwa alitumia fursa hiyo kumnasa Kuria kujiunga na Azimio La Umoja katika azma ya kuifanya Kenya kuwa nchi bora.

"Nzuri kukutana na kaka yangu Mhe. Moses Kuria akiwa Dubai na nimefurahi kushuhudia kupona kwake. Nimemwomba ajiunge na timu ya ushindi Azimio, tupeleke Kenya mbele pamoja," alisema Jumanne.

Wawili hao walikutana katika Kongamano la Baraza la Ushirikiano la Ghuba-Kenya Biashara linalotarajiwa kufunguliwa na Rais Uhuru Kenyatta baadaye Jumanne.

Mnamo Februari 3, Naibu Rais William Ruto pia alimtembelea Mbunge wa Gatundu Kusini katika hospitali ya Dubai.