Mume aliyefukuzwa na mkewe baada ya kuishi pamoja miaka 25 apata haki mahakamani

Pia atafaidika na kodi iliyokusanywa kutoka kwa majengo hayo tangu alipopigwa teke nje mwaka 2011.

Muhtasari

• Mwanamume huyo alieleza kuwa mali hiyo ilisajiliwa kwa jina la mwanamke huyo kwa sababu mmiliki wake hakuridhika kumuuzia kwa vile hakuwa wa kabila la muuzaji.

Mahakama
Mahakama

Ni afueni kwa mwanamume mfanyibiashara wa Nairobi aliyefukuzwa na mke wake kutoka kwa nyumba baada ya kuishi pamoja kwa miaka 25.

Kwa mujibu wa ripoti ya NTV Kenya, mwanamume huyo alielekea mahakamani na hatimaye amepata haki baada ya korti kuamuru kwamba anastahili kupata mgao wa asilimia 30 ya mali waliyotengeneza pamoja katika kipindi hicho cha robo karne.

Mwanamume huyo anayejulikana kwa jina la POM ili kulinda utambulisho wake sio tu kwamba atakusanya kodi kutoka kwa nyumba 11 kati ya 38 za biashara na makazi zinazojumuisha chumba kimoja na vyumba viwili vya kulala na duka lakini pia atafaidika na kodi iliyokusanywa kutoka kwa majengo hayo tangu alipopigwa teke nje mwaka 2011.

Jaji wa Mahakama ya Juu Hillary Chemitei aliamuru utiifu wa uamuzi wa Mahakama ya Juu uliompa mwanamume huyo asilimia 30 ya mali.

"Sidhani kwamba kile POM inauliza ni kati ya haki yake ya asilimia 30 katika mali ya suti. Anafaa kuruhusiwa kufurahia vile vile,” hakimu alisema katika uamuzi wake kama ulivyonukuliwa na NTV Kenya.

Mwanamume huyo alikuwa ameanzisha kesi dhidi ya mwanamke huyo ambaye alidai kuwa mke wake.

Alidai kuwa walianza kuishi pamoja kama mume na mke mwaka wa 1986 na kwamba kutokana na akiba ya pamoja, walinunua mali ambayo baadaye iligeuka kuwa mzozo baada ya kufukuzwa.

Mwanamume huyo alieleza kuwa mali hiyo ilisajiliwa kwa jina la mwanamke huyo kwa sababu mmiliki wake hakuridhika kumuuzia kwa vile hakuwa wa kabila la muuzaji.