- Kuzima akaunti yake ya Twitter kulikuwa baada ya vita vya maneno kati yake na Wakili Donald Kipkorir kuhusu Uchaguzi Mkuu wa 2022
Msemaji wa Azimio la Umoja Makau Mutua amewataka Wakenya kukoma kumshambulia Winnie Odinga bintiye bosi wa ODM Raila Odinga.
Katika taarifa yake Jumatano, Mutua alisema Winnie ni mwanasiasa mchanga na anafaa kuelimishwa.
"Wale ambao wamekuwa wakimshambulia Winnie Odinga wakome na waache. Yeye ni mwanamke mchanga katika siasa. Mwanamume amabye yuko kwenye hali yake hatakuwa mjanja sana. Winnie alipata talanta, lakini ushauri utakuwa muhimu. Tuwaunge mkono vijana wetu," Mutua alisema.
Hii ni baada ya Winnie Odinga kurejea kwenye Twitter baada ya mwezi mmoja wa kuzima akaunti yake.
"Nimerudi kwenye Twitter baada ya muda na kutajwa kwangu kumevurugika. Naona umekuwa ukizungumza. Ila ujue kuna mfumo tofauti kabisa kati ya kampeni za uchaguzi na siku ya uchaguzi. Ningekuwa nashughulikia hili ningekuwa naandika kwenye kutoka kwenye ukumbi wa harusi! " aliandika Winnie baada ya kurejea Twitter.
Those who’ve been attacking @Winnie_Odinga should CEASE and DESIST. She’s a young woman in politics. A man in her shoes wouldn’t be so pilloried. Winnie got talent, but advice and mentorship will be key. Let’s support our young, not “eat” them.
— Prof Makau Mutua (@makaumutua) October 19, 2022
Kuzima akaunti yake ya Twitter kulikuwa baada ya vita vya maneno kati yake na Wakili Donald Kipkorir kuhusu Uchaguzi Mkuu wa 2022.
Wakili huyo alikuwa amedai kuwa Winnie alikuwa miongoni mwa timu ya Azimio iliyohujumu uchaguzi wa Raila wa Agosti 9.