- Ruto asema mkutano huo sasa utaandaliwa alhamisi wiki ijayo
- Awali polisi waliwatawanya wafuasi wake huko Nyamira
- Hayo yanajiri siku moja baada ya baraza la ushauri la usalama wa kitaifa kutoa taarifa kali ya kukemea kampeini za kisiasa wakati huu
Naibu wa rais William Ruto ameahirisha ziara yake ya kwenda Nyamira baada ya polisi kuwatawanya wafuasi wake kutumia vitoa machozi
Ruto ametumia twitter kuwashambulia polisi kwa kuvuruga mkutano wa Amani . amesema baada ya kushauriana na wabunge Kemosi, Mose,Nyamoko, chama cha boda boda na viongozi wa makanisa waliokuwa wamemualika huko Nyamira mkutano huo sasa utafanyika alhamisi wiki ijayo.
After consultations with MPs Kemosi, Mose,Nyamoko, the bodaboda sacco and church leadership who had invited us, we have postponed the two functions in Nyamira County to Thursday next week.The disruptive dispersal by police of kenyans engaged in economic empowerment is unnecessary
— William Samoei Ruto, PhD (@WilliamsRuto) October 8, 2020
Amesema polisi hawafai kuvuruga mkutano unaolenga kuwahamasisha kiuchumi wakenya
Awali polisi katika kaunti ya Nyamira waliwaamrisha wananchi kutoka katika uwanja wa shule ya upili ya Keberigo ambako mkutano mmoja wa Ruto ulitarajiwa kufanywa .
Polisi walifika katika uwanja huo na kuitaka bendi ya muziki iliyokuwa ikiendelea na kuwatumbuiza wananchi kuondoka wakisema hakuna mkutano ambao ungefanyika katika shule hiyo .
Tayari kundi la Ruto lilikuwa limeshafika katika maeneo yote ya mikutano yake kabla ya kuwasili kwake kwa sabau alikuwa amehudhuria mkutano wa baraza la mawaziri Nairobi .
Tulizungumza wiki jana na kamishna wa kaunti kuhusu mkutano wetu na akakubali ,sasa kwa bahati mbaya ameamua kuuvurug’ amesema mbunge Kemosi