'Kama nimekukosea nisamehe ,na mimi wale wamenekosea nimewasamehe'

Uhuru aomba msamaha ,akisema pia amewasamehe waliomkosea

Rais Uhuru ndiye mwanasiasa aliyetoa houtuba katika hafla hiyo ya maombi

Muhtasari

 

  •  Uhuru aliomba msamaha kwa kupata na hasira na kuwafokea viongozi waliokuwa wamemshambulia kwa maneno
  • Amesema  msamaha na maridhiano ndio njia pekee ya kulipeleka taifa mbele 

 

 

Rais Uhuru Kenyatta

 

  Rais Uhuru Kenyatta  siku ya jumamosi  alionekana kulegeza   kamba kuhusu  maridhiano ya kitaifa wakati wa hafla ya maombi iliyohusisha madhehebu mbali mbali katika Ikulu ya Nairobi .

Uhuru aliwaomba msamaha watu ambao amewakosea na pia kusma kwamba amedwasamehe waliomkosea .Amesema ni kupitia  maridhiano ambapo taifa linaweza kuafikia umoja .

“  Mimi nasema kama nimekukosoa basi nisamehe na mimi nimewasamehe wale wamenikosea’ Uhuru amesema .

 Rais Kenyatta hivi maajuzi amekuwa katika mgongano na baadhi ya wabunge hasa kutoka mrengo wa  tanga tanga waliotumiwa matusi na lugha isiofaa dhidi yake na familia yake .

  Mwezi Uliopita  Uhuru ambaye alikuwa na ghadhabu baada ya kushambuliwa na viongzi hao alifoka kwa hamaki na pia akatupia cheche kali za maneno kwa kuwaita ‘wajinga’ huku akiwashauri wawashambulie mama zao na sio wake .

 “ Hii ndio njia pekee ya kupeleka Kenya mbele ,Amani ,Amani  ili tuwe pamoja kama wakenya’ amesema rais

 Katika hafla hiyo iliyohudhuriwa pia na  naibu wa rais William Ruto ,rais Kenyatta ndiye mwanasiasa pekee aliyetoa hotuba kwa ajili ya kuwa mwenyeji .

Wengine waliohudhuria hafla hiyo ni   mke  rais Mama Margaret Kenyatta ,kiongozi wa Wiper  Kalonzo Musyoka ,Kiongozi wa ANCMusalia Mudavadi maspika wa mabunge yote  Justin Muturi na  Ken Lusaka miongoni mwa wengine .