- Amewataka wakaazi kuisima ripoti ya BBI
- Rais amekagua miradi mbali mbali ya amendeleo mjini Kisumu
Rais Uhuru Kenyatta siku ya alhamisi amepokelewa kwa kishindo mjini kisumu na wakaazi waliojitokeza kumtazama alipokuwa akikagua miradiu ya maendeleo .
Wakaazi walibeba mabango ya kumsifia rais uhuru Kenyatta na kiongozi wa ODM Raila Odinga walipokuwa wakipigia debe ripoti iliyotolewa jana ya BBI .
Alipowasili kondele rais alilazimika kutoka nje ya gari lake kuwaamkua wananchi waliokuwa wakimshangilia .
Umati wa wa watu wakiwemo boda boda ulianza kufuata msafara wa rais hadi katika uwanja wa Mamboleo Showground ambapo rais aliweka jiwe la msingi kwa ujenzi wa uwanaj wa kimataifa wa michezo wa Jomo Kenyatta
Wakaazi walionyesha furaha yao kwamba rais alichukua hatua ya kuwaamkua baada ya kufadhaishwa jana wakati alipotua katika bandari ya Kisumu badala ya uwanja wa ndege ambako walikuwa wamemngoja .