- Watu 957 wamepatikana na virusi vya corona baada ya sampuli 5,559 kupimwaLeo watu 2,616
- wamepona na kufikisha 49,878 idadi ya watu waliopona corona nchini
Watu 957 wamepatikana na virusi vya corona baada ya sampuli 5,559 kupimwa katika saa 24 zilizopita na kufikisha 72,686 idadi ya visa v vya corona vilivyothibitishwa nchini huku idadi ya sampuli zilizopimwa ikifikia 804,894.
Kutoka visa hivyo vipya 908 ni wakenya ilhali 49 ni raia wa kigeni .wagonjwa 569 ni wanaume huku 388 wakiwa wanawake .Mgonjwa wa umri wa chini kupatikana na ugonjwa huo ni mtoto wa miezi miwili ilhali wa umri wa juu ana miaka 94 .
Leo watu 2,616 wamepona na kufikisha 49,878 idadi ya watu waliopona corona nchini
Hata hivyo watu 11 wameaga dunia na kufikisja 1,313 idadi ya walioangamizwa na corona hadi kufikia sasa . wagonjwa 1,191 wamelazwa katika hospitali mbali mbali ilhali 6000 wapo chini ya utunzi wa nyumbani . wagonjwa 58 wapo katika kitengo cha ICU .
Hadi kufikia leo wafanyikazi 2,369 wa afya wamepatikana na corona huku 30 wakiafa dunia .