- Mbunge huyo alitaka kupewa siku 90 akisema ana virusi vya Covid 19
- Kesho ndio makataa ya Barasa kulipa shilingi milioni 1.8
Mbunge wa Kimilili Didmus Barasa ana hadi siku ya jumanne kumlipa wakili mmoja jijini Nairobi shilingi milioni 1.8 au apelekwe jela kwa miezi sita
Barasa anadaiwa na wakili Alfred Ndambiri kwa gharama ya huduma za kumwakilisha katika kesi ya kuinga kuchaguliwa kwake iliyowasilshwa dhidi yake na mbunge wa zamani wa Kimilili Suleiman Murunga mwaka wa 2017
Wakili huyo amekuwa akimdai Barasa p[esa zake tangia wakati huo hadi alipoamua kuwasilisha kesi kwa hakimu D.M Kivuti .
Barasa alikuwa ametaka kupewa muda Zaidi ili kuzilipa fedha hizo na mara ya mwisho hakimu alikuwa ametoa agizo Barasa kufika mbele yake Novemba tarehe 24 .
Kivuti aliamuru kwamba iwapo hatokuwa amelipa fedha hizo basi atahudumu kifungo cha miezi sita jela . Barasa awali alitaka kupewa siku 90 kwa sababu alisema alikuwa amepatikana na COVID 19 na alikuwa amejitenga .Jaji hata hivyo alimpa siku 45 zinazokamilika kesho