Mashakani

Korti yaagiza kukamatwa kwa mbunge Didmus Barasa kuhusu deni la milioni 1.8

Barasa anadaiwa na wakili shilingi milioni 1.8

Muhtasari

 

  •  Mbunge huyo alikuwa amepewa hadi siku ya jumanne kulipa deni hilo 
  •  Hata hivyo Barasa amekosa kufika kortini leo na waranti ya kukamatwa kwake imetolewa 

 

Mbunge wa Kimilili Didmus Barasa

Mahakama moja ya Nairobi imeagiza kukamatwa kwa mbunge wa kimilili Didmus Barasa kuhusu kukosa kulipa deni  la shilingi milioni 1.8   na huenda akahudumia kifungo cha miezi sita jela

 Hakimu  DM Kivuti  wa mahakama ya milimani jumanne  aliagiza  kwamba waranti ya kukamatwa kwa mbunge huyo ikabidhiwe OCS  wa kituo cha polisi cha Central Nairobi kwa hatua .

Barasa  alikuwa na hadi siku y jumanne kumlipa wakili Afrd Ndambiri deni lake la shilingi milioni 1.8 au ahudumie kifungo cha miezi sita jela . Mbunge huyo hata hivyo hajafika kortini   leo .

Barasa  anadaiwa na Ndabiri fedha hizo kama ada ya kumwakilisha katika kesi ya kupinga kuchaguliwa kwake iliyowasilishwa kortini na mbunge wa zamani wa Kimilili Suleiman Murunga mwaka wa 2017

 Baada ya kumdai kwa muda mrefu ,wakili huyo alilazimika kumshatki Barasa kortini na kesi hiyo kuwasilishwa mbele ya hakimu D.M Kivuti .

 Katika vikao vingine  mara saba wakati  Barasa alipofika mbele ya hakimu alidai kupewa muda zaidi akiadi kulipa deni hilo lakini hakufanya hivyo .