- Polisi na walishuhudia tukio hilo wanasema kizaazaa kilianza wakati Constable Lawrence Ewoi alipoanza ugomvi na Achieng kuhusu sababu isiojulikana nje ya kituo hicho.
- Ugomvi huo ulimfanya Ewoi aliyekuwa amejihami kwa bunduki ya G3 kurudi nyuma na kumpiga risasi mwenzake aliyekuwa ndani ya gari . Alifyatua risasi takriban nne zilizompiga Achieng kifuani .
Afisa mmoja wa polisi ameuawa na wenzake kwa kupigwa risasi saa chache baada yay eye kumwuua mwenzake kwa kumpuiga risasi pia katika eneo la Kamukunji ,Nairobi
Afisa mwingine wa polisi alijeruhiwa kwa kupigwa risasi mkononi katika patashika hiyo .Tukio hilo limefanyika jumamosi mwendo wa saa unusu usiku .
Mwathiriwa wa kwanza alikuwa Constable Maureen Achieng aliyepigwa risasi na kuuawa ndani ya gari la polisi wakati yeye na wenzake walipokuwa wakijitayarisha kwenda kupiga doria za usiku .
Polisi na walishuhudia tukio hilo wanasema kizaazaa kilianza wakati Constable Lawrence Ewoi alipoanza ugomvi na Achieng kuhusu sababu isiojulikana nje ya kituo hicho.
Ugomvi huo ulimfanya Ewoi aliyekuwa amejihami kwa bunduki ya G3 kurudi nyuma na kumpiga risasi mwenzake aliyekuwa ndani ya gari . Alifyatua risasi takriban nne zilizompiga Achieng kifuani .
Risasi hizo pia zilimpata Constable George Gitonga katika mkono wake wa kushoto .
“ Hawakuweza kujibu shambulizi hilo kwa sababu walikuwa ndani ya gari na katika nafasi iliyojibana huku polisi huyo akiwafyatulia risasi’ amesema shahidi mmoja
Polisi wanasema Achieng alitajwa kuwa amefariki alipokimbizw akatika hospitali ya kitaifa ya Kenyatta ilhali Gitonga amelazwa akiwa katika hali thabiti .
Wakati polisi waliojeruhiwa walipokuwa wakikimbizwa hospitali mshukiwa Ewoi alikwepa eneo la tukio . Wenzake walisambaza maelezo yake katika redio za polisi na kuonya kwamba alikuwa amevalia nguo za raia akiwa amejihami .
Msako mkubwa ulianzishwa dhidi yake kwa saa moja kabla ya kupatwa na kuuawa karibu na soko la Burma ambapo alikuwa amebadiliusha nguo zake na alipanga kurejea kituoni . Alipatikana na bunduki aliotumia kutekeleza mauaji ya Achieng . Ewoi alikuwa akifanya kazi katika kikosi malaum cha QRU kilichokuwa na jukumu la kujibu visa vya uhalifu kwa dharura
Mkuu wa polisi Nairobi Rashid Yakub amesema hawajajua chanzo cha mauaji hayo ya kwanza
“ Tumewapoteza maafisa wawili wazuri katika hali ya bahati mbaya . Tunachunguza kiini cha matukio haya .Miili imepelekwa katika hifadhi ya maiti .