BBI

Raila kuandaa kikao cha BBI Kisumu baada ya mkutano wa Uhuru Sagana

Mkutano huo pia utawahusisha waakilishi wa kibiashara na wazee wa jamii ya Waluo , Tayari mialiko imetumwa kwa takriban watu 800 .

Muhtasari
  •   Mkutano huo wa Raila utafayioka wiki moja baada ya rais Kenyatta kuandaa mkutano Sagana na viongozi kutoka mlima Kenya kuwashawishi waunge mkono mswada wa BBI .
  • Katika mkutano wa Kisumu  Raila atakutana na  magavana wote ,wabunge ,wataalam na waakilishi wa mabunge ya kaunti kutoka  Migori, Homabay, Kisumu  na Siaya.

 

Kiongozi wa ODM Raila Odinga

Rais Uhuru Kenyatta  na kiongozi wa ODM Raila Odinga wameamua kurejea katika ngome zao kupigia debe ripoti ya BBI baada ya  mswada wa BBI kuidhinishwa na tume ya uchaguzi nchii IEBC .

 Kiongozi  huyo wa ODM  anapanga kufanya mkutano mkubwa na washika dau katika sekta mbali mbali  kutoka kaunti nne za Luo Nyanza februari tarehe 8  huku BBI ikitarajiwa kuwa ajenda kuu .

 Mkutano huo wa Raila utafayioka wiki moja baada ya rais Kenyatta kuandaa mkutano Sagana na viongozi kutoka mlima Kenya kuwashawishi waunge mkono mswada wa BBI .

Uhuru  amekuwa katika eneo la kati tangu siku ya ijumaa  katika kile ambacho ikulu imetaja kama ziara ya kikazi na  ya kukutana na viongozi waliochaguliwa kutoka eneo hilo ili kujadili BBI na masuala mengine yanayohusu maendeleo .

 Katika mkutano wa Kisumu  Raila atakutana na  magavana wote ,wabunge ,wataalam na waakilishi wa mabunge ya kaunti kutoka  Migori, Homabay, Kisumu  na Siaya.

 Mkutano huo pia utawahusisha waakilishi wa kibiashara  na wazee wa jamii ya Waluo , Tayari mialiko imetumwa kwa takriban watu 800  .