Wachuuzi wa ngono UK wandamana kupinga mauji ya Agnes Wanjiru

Muhtasari

•Wachuuzi wa ngono nchini Uingereza waliandamna dhidi ya mauaji  ya Agnes Wanjiru yanayodaiwa kutekeleze na  mwanajeshi wa Uingereza.

Mnamo Desemba 17, makundi ya wachuuzi wa ngono yalikusanyika nje ya afisi ya Wizara ya Ulinzi ili kutaka haki itendeke kwa Wanjiru.
Mnamo Desemba 17, makundi ya wachuuzi wa ngono yalikusanyika nje ya afisi ya Wizara ya Ulinzi ili kutaka haki itendeke kwa Wanjiru.
Image: Twitter/Kiingereza Mkusanyiko wa Makahaba

Wachuuzi wa ngono afanyabiashara wa ngono  katika nchi ya Uingereza wameandamana kufuatia madai ya mauji  ya Agnes Wanjiru na  mwana jeshi wa Uingereza.

 Mnamo Disemba 17, Makundi ya mahakaba  yalikusanyika nje ya afisi ya Wizara ya Ulinzi ili kuitaka haki itendeke kwa Wanjiru 

Muungano wa Uingereza wa Makahaba, Kundi la Wanawake wote wa Afrika, lile la Wanawake dhidi ya Ubakaji, SWARM, walikuwa miongoni mwa makundi yaliyotaka haki itendeke kwa Agnes na wafanyakazi wengine ambao sauti zao hazikusikika.

"Tunawaheshimu na kuwaomboleza wahudumu wa biashara ya ngono duniani kote ambao wamekuwa wahasiriwa wa dhuluma na mauaji. Leo pia ni siku ya upinzani - tuko nje ya Wizara ya Ulinzi kutoa wito wa haki kwa Agnes Wanjiru, mchuuzi fanyakazi wa ngono wa Kenya na mama aliyeuawa na afisa wa Jeshi la Uingereza,"  baadji ya mahakaba wa Uingereza waliandika kwa mtandao wao wa twitter.

Waandamanaji walibeba bendera, mabango  na miavuli vikiwa na sheheni maneno yenye kuonyesha kughadhabishwa kwao na mauaji ya Wanjiru.

Mwili wa Wanjiru ulipatikana katika  Lion court Hotel, Nanyuki baada ya miezi mbili ya kutafutwa.