Wakenya wengi wanaamini uchaguzi wa rais utakuwa wa huru na wa haki- TIFA

Muhtasari

•Asilimia 20 wanaamini kuwa hakutakuwa na wizi wa kura ilhali asilimia 10 hawana uhakika.

Mchanganuzi wa siasa Tom Wolf akihutubia waandishi wa habari kuhusiana na utafti wa BBI jijini Nairobi mnamo Julai 1,2021
Mchanganuzi wa siasa Tom Wolf akihutubia waandishi wa habari kuhusiana na utafti wa BBI jijini Nairobi mnamo Julai 1,2021
Image: Charlene Malwa

Wakenya wengi wanaamini kuwa uchaguzi wa urais wa Agosti 9 utakuwa huru na wa haki, utafiti wa TIFA unasema.

Utafiti huo unasema asilimia 37 ya Wakenya wana uhakika kuwa kutakuwa na uwazi katika uchaguzi wa mwaka huu.

Haya ni licha  ya naibu Rais William Ruto ambaye ni mmoja wa wanaowania kiti cha urais kusema kuna uwezekano wa kura hizo kuibiwa.

Image: TIFA

Utafiti huo hata hivyo ulibainisha kuwa asilimia 32 ya Wakenya wanaamini kwa kiasi fulani kuwa uchaguzi huo utaibiwa.

Image: TIFA

Asilimia 20 wanaamini kuwa hakutakuwa na wizi wa kura ilhali asilimia 10 hawana uhakika.