Muhtasari
•Jumba moja liliporomoka katika eneo la Infinity eneo la Mwiki Estate, eneo la Kasarani jijini Nairobi Jumatano jioni.
Jumba moja liliporomoka katika eneo la Infinity eneo la Mwiki Estate, eneo la Kasarani jijini Nairobi Jumatano jioni.
Timu ya St John Ambulance imekimbia katika eneo la tukio katika juhudi za uokoaji. Hakuna waathiwa wowote ambao wameripotiwa kufikia sasa.
"Timu zetu za kukabiliana na dharura zikikimbilia eneo la tukio. Taarifa zaidi zitafuata hivi punde," St John Ambulance ilisema kupitia Twitter.
Jengo la ghorofa nne lililoporomoka lilikuwa ni nyumba ya kupangisha.
Polisi wamesema kuwa shughuli za uokoaji bado zinaendelea. Kikosi cha Kenya Red Cross pia kimeonekana katika eneo la tukio.
Mengine yanafuata...