Kobe liaga dunia pamoja na bintiye mwenye umri wa miaka 13 Gianna na watu wengine wanane.
Kobe na mkewe wamekuwa katika ndoa tangu mwaka wa 2001 na kulingaa na jarida moja la People mkewe hakupendelea kusafiri naye katika helikopta. Kobe mweye umri wa miaka 41 alikuwa tu akimtumia rubani mmoja Ara Zobayan ambaye pia aliaga dunia katika ajali hiyo ya siku ya jumapili. Kobe awali amewahi kuzungumza kuhusu mapenzi yake ya kutumia helikopta ili kuepuka msongamano wa magari alipokuwa akiichezea timu ya Los Angeles Lakers.
Kobe alikuwa akielekea katika chuo chake cha mafunzo ya mchezo wa vikapu cha Mamba Sports Academy kwa mchuano wa vijana pamoja na binti yake Gianna, alikuwa pia na mama na binti Sarah na Payton Chester, kocha wa timu ya wasichana ya mchezo wa vikapu Christina Mauser, kocha mmoja wa mchezo huo shuleni John Altobelli na mkewe Keri pamoja na binti yao Alyssa, wakati ndege hiyo ya helikopta ilipoanguka katika milima Calabasas iliyojaa ukungu . Amemwacha mkewe Vanessa mwenye umri wa miaka 37 na binti zao Natalia, 17, Bianka, 3, na Capri, aliyezaliwa Juni 2019.