Michael Joseph ateuliwa mwenyekiti wa bodi ya Safaricom

MJ
MJ
Safaricom imemetaua Michael Joseph kuwa mwenyekiti mpya wa bodi yake . Anaichukua nafasi hiyo kutoka kwa Nicholas Ng’ang’a ambaye anastaafu baada ya kuiongoza bodi ya kampuni hiyo kwa miaka 16 .

Safaricom itatoa tangazo hilo rasmi kwa umma wakati wa mkutano wake wa kila mwaka   siku ya alhamisi.

mwenyekiti wa bodi ana jukumu la kusimamia oparesheni na uongozi wa  bodi  ili kuunda ajenda ifaayo kwa ufanisi wa kampuni hiyo .

Michael Joseph ndiye afisa mkuu mtendaji wa kampuni hiyo ,nafasiambayo aliishikilia kuanzia  julai mwaka wa 2019 hadi machi mwaka wahuu . Alijiunga na  kampuni hiyo septemba tarehe 8 mwaka wa 2008 .

Awali aliwahi kuwa afisa mkuu mtendani wa safaricom  kuanzia julai mwaka wa 2000  wakati kampuni hiyo ilipozinduliwa upya kama biashara ya pamoja ya  Vodafone UK  na Telkom Kenya  hadi alipostaafu novemba mwaka wa 2010.