Kipchoge awa mwanariadha wa kwanza kuwahi kushinda Berlin Marathon mara 5

Kipchoge sasa anakuwa mwanariadha wa kwanza kushinda mbio za Berlin Marathon mara tano. Ndiye anayeshikilia rekodi ya dunia ya marathon kwa sasa, ambayo alikuwa ameweka kwa muda wa kumaliza wa 2:01:09.

Muhtasari

• Ushindi wa tano wa Kipchoge unamshinda Muethiopia Haile Gebrselassie ushindi wa nne.

• Mkenya mwingine Vincent Kipkemboi aliibuka wa pili baada ya kutumia saa 2:03:13.

Elidu Kipchoge.
Elidu Kipchoge.
Image: Hisani

Mshikilizi wa rekodi ya dunia kutoka Kenya Eliud Kipchoge ameshinda mbio za Berlin Marathon kwa mara ya tano, akivuka mstari katika muda wa saa 2 dakika 02 na sekunde 42 katika mji mkuu wa Ujerumani siku ya Jumapili.

Kipchoge alipovuka msitari wa kumalizia, kiongozi wa wanawake Tigist Assefa alikuwa dakika tatu mbele ya rekodi ya awali ya dunia ya saa 2:14:04, hivyo kumfanya aendelee kutinga hatua hiyo.

Ushindi wa tano wa Kipchoge unamshinda Muethiopia Haile Gebrselassie ushindi wa nne.

Mkenya mwingine Vincent Kipkemboi aliibuka wa pili baada ya kutumia saa 2:03:13.

Tadese Takele wa Ethiopia aliibuka wa tatu akitumia saa 2:03:24. Wawili hao ni washiriki wa kwanza wa Berlin Marathon.

Kipchoge sasa anakuwa mwanariadha wa kwanza kushinda mbio za Berlin Marathon mara tano.

Ndiye anayeshikilia rekodi ya dunia ya marathon kwa sasa, ambayo alikuwa ameweka kwa muda wa kumaliza wa 2:01:09.

Kabla ya mbio hizo, Kipchoge alisema kuwa lengo lake kuu ni kushinda medali tatu za dhahabu za Olimpiki mfululizo na kwamba anaamini kukimbia mjini Berlin ndiyo njia bora ya kujiandaa kwa hili.

Kipchoge, bingwa mara mbili wa Olimpiki kutoka Kenya, alikuwa anawinda ushindi wake wa tano katika mbio za wanaume mjini Berlin.

Alivunja rekodi ya dunia kwa nusu dakika kwa muda wa 2:01:09 mjini Berlin mwaka jana, ukiwa ni ushindi wake wa nne. Awali Kipchoge alishinda Berlin Marathon mwaka wa 2015, 2017, na 2018, akiweka rekodi ya dunia ya saa 2:01:39 mwisho.

Akizungumzia kurejea kwake Berlin, Kipchoge alisema, "Berlin, kwangu mimi, ni kama nyumbani. Nikiangalia Michezo ya Olimpiki mjini Paris mwaka ujao, nilizingatia mbio zipi zingekuwa maandalizi bora kwangu, na Berlin ilikuwa chaguo bora zaidi."

Kipchoge, mmoja wa wanariadha wakubwa zaidi katika historia, amepoteza mara tatu pekee katika mbio za marathoni 18 alizokimbia. Atakabiliana na ushindani mkubwa, akiwemo mwenza wake Amos Kipruto, ambaye alimaliza wa pili kwa Kipchoge katika mbio za Tokyo Marathon mwaka jana.