Arturo Vidal anamsuta kocha Erik ten Hag akisema 'watu wenye vipara wamechanganyikiwa'

Arturo Vidal amemdhihaki Erik ten Hag kwa upara wa kichwa huku akikosoa kazi aliyoifanya Manchester United - na jinsi alivyowafanyia Cristiano Ronaldo, Mason Greenwood na sasa Jadon Sancho.

Muhtasari

• Ten Hag alipoteza nywele wakati wa kucheza mwaka 1996 - lakini alikuwa amenyoa kichwa chake muda mrefu kabla ya kazi yake ya ukocha kuanza mwaka wa 2011.

Vidal na Ten Hag
Vidal na Ten Hag
Image: X

Mchezaji wa zamani wa Barcelona na timu ya taifa ya Chile, Arturo Vidal amemkashifu upara wa kichwa cha meneja wa Manchester United Erik ten Hag huku akimsuta kwa jinsi anavyowafanyia wachezaji.

Vidal, ambaye anajulikana sana kwa muda wake wa kukaa Juventus, Bayern Munich na Barcelona, ​​alitoa mawazo yake kuhusu kocha huyo wa zamani wa Ajax mtandaoni.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 36 ambaye alijiunga na Athletico Paranaense kutoka Flamengo msimu wa joto, alikosoa sana jinsi Ten Hag amewafanyia wachezaji kama Christiano Ronaldo, Mason Greenwood na wa hivi karibuni Jadon Sancho.

Vidal alisema kuhusu ujio wa Ten Hag United wakati wa mtiririko wa moja kwa moja: "Kocha huyo aliingia vibaya. Utamtoaje Cristiano Ronaldo?" Kisha akaongeza: "Ndivyo walivyo hawa. Alikuwa mfungaji bora na anamtoa nje. Mameneja wenye vipara ni watu waliochanganyikiwa sana."

Msimamo wa Vidal juu ya mabosi wenye vipara huenda ulitokana na wakati alipokuwa Flamengo chini ya bosi wake wa zamani wa Chile Jorge Sampaoli, ambaye kiungo huyo alimtaja kuwa hafai baada ya kuondoka kwake.

Ten Hag alipoteza nywele wakati wa kucheza mwaka 1996 - lakini alikuwa amenyoa kichwa chake muda mrefu kabla ya kazi yake ya ukocha kuanza mwaka wa 2011.

Inashangaza kwamba Vidal anachagua kunyoa sehemu kubwa za kichwa chake akiwa na kipara kabisa huku akiacha mohican nyembamba ambayo anapaka rangi kama blonde.

Ten Hag aliamua kumuondoa Ronaldo kwenye benchi alipowasili Old Trafford kabla ya kukubaliana kwamba mkongwe huyo wa zamani wa Real Madrid anaweza kufuta kandarasi yake na kujiunga na Al-Nassr kwenye Ligi Kuu ya Saudia.

Baadae piaaliweza kuonekana wazi kumtoa kweney timu hiyo kinda Mason Greenwood kufuatia sakata la kesi ambayo ilikuwa inamkabili kabla ya kujiunga na Getafe msimu wa joto.

Hivi karibuni, Ten Hag amekuwa akisumbuana na kinda Jadon Sancho baada ya kudai kwamba hakumuorodhesha kwenye kikosi kilichochabangwa na Arsenal kisa uzembe wake.

Sancho alikwenda mitandaoni na kukana vikali madai ya uzembe akisema kwamba amechoka kilimbikiziwa lawama ambazo si za kweli.

Ten Hag alimuondoa kwenye timu ya kwanza na kiungo huyo kutakiwa kuomba radhi kwa matamshi yake - jambo amblo amedinda kulifanya.

Shukrani kwa Vidal, bosi wake mlezi wa sasa Wesley Carvalho huko Paranaense ana nywele kamili, kama vile meneja wa Chile Eduardo Berizzo.