Rodri wa Man City amchagua Morata wa Atletico kama straika bora kuliko Haaland

Alvaro Morata amekuwa akifurahia kiwango kizuri katika kampeni ya sasa. Kulingana na Transfermarkt, ana michango 15 ya mabao (mabao 12 na asisti tatu) katika michezo 15 katika mashindano yote.

Muhtasari

• Katika msimu huu kwenye mashindano yote, Haaland ameshiriki katika mechi 18 na kufunga mabao 17, kwa mujibu wa TransferMarket.

Rodri.
Rodri.
Image: X

Kiungo wa kati wa Manchester City na timu ya taifa ya Uhispania, Rodri amefunguka kuhusu mshambuliaji bora ambaye amewahi kucheza na yeye.

Rodri ambaye yuko kambini kuitumikia Uhispania katika michuano ya kimataifa alikuwa anazungumza na gazeti la Mundo Deportivo nchini humo wakati aliulizwa kati ya washambuliaji Earling Haaland wanayecheza na yeye Manchester City na Alvaro Morata wa Atletico Madrid wanayecheza na yeye timu ya taifa nani bora katika ufungaji mabao.

Mchezaji huyo wa kiungo aliharakisha kuashiria ubora endelevu wa Morata, akisisitiza uchezaji thabiti wa mshambuliaji huyo msimu baada ya msimu.

"Ni wazi, Morata," alisema akinukuliwa na Mundo Deportivo. "Ukweli ni kwamba nina bahati sana kucheza nao. Álvaro amekuwa akifanya vyema katika timu ya taifa kwa miaka mingi. Yupo juu na wababe wa historia yetu katika idadi ya mabao, na hakuna cha kusema kuhusu Erling kwa sababu ana kila kitu mbele yake kuwa mmoja wa bora."

Kwa kulinganisha, Alvaro Morata amekuwa akifurahia kiwango kizuri katika kampeni ya sasa. Kulingana na Transfermarkt, ana michango 15 ya mabao (mabao 12 na asisti tatu) katika michezo 15 katika mashindano yote.

Mshambulizi huyo wa Manchester City amekuwa akifunga kwa kufurahisha kufuatia kuhamia kwake Ligi ya Premia na kumaliza kampeni za 2022-23 kama mfungaji bora, na kuvunja rekodi nyingi.

Katika msimu huu kwenye mashindano yote, Haaland ameshiriki katika mechi 18 na kufunga mabao 17, kwa mujibu wa TransferMarket.