Harry Maguire amemtaja Neymar Jr kama mchezaji aliyempa taabu sana kumkaba

Maguire alikutana na Neymar kwa mara ya kwanza kwenye Ligi ya Mabingwa wakati Manchester United ilipokuwa dhidi ya Paris Saint Germain mnamo Desemba 2 2020.

Muhtasari

• Neymar aliishia kufunga mabao mawili huku Mashetani Wekundu wakikubali kichapo cha 3-1 katika mchezo ambao kiungo Fred alitolewa nje kwa kadi nyekundu.

• Neymar kwa sasa anauguza jeraha ambalo limemaliza msimu wake.

Harry Maguire na Neymar.
Harry Maguire na Neymar.
Image: X

Aliyekua nahodha wa Manchester United kabla ya kuvuliwa unahodha, Harry Maguire alikuwa na jibu la kuvutia alipoulizwa kumtaja mpinzani wake mgumu zaidi kuwahi kutokea.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 30 amemenyana dhidi ya baadhi ya wachezaji bora katika biashara, hasa kwa sababu amecheza Ligi ya Premia kwa miaka.

Tangu enzi zake akiwa Leicester City, Maguire amekuwa akikabiliana na magwiji wa kisasa wa mchezo huo, akiwemo Eden Hazard, Harry Kane, Kevin de Bruyne na Sergio Aguero, lakini mchezaji mmoja anashika nafasi ya juu ya majina haya yote kwa upande wa beki wa kati.

Katika kipindi cha hivi majuzi cha Maswali na Majibu na JD Football, Maguire alifichua kuwa fowadi wa Al Hilal Neymar ndiye mpinzani mbaya zaidi ambaye amewahi kukumbana nayo.

“Mpinzani wangu mgumu zaidi ni Neymar. Nilicheza dhidi yake PSG na Brazil pale Wembley. Ni mpinzani mkali; ni ngumu kuweka alama,” alisema.

Maguire alikutana na Neymar kwa mara ya kwanza kwenye Ligi ya Mabingwa wakati Manchester United ilipokuwa dhidi ya Paris Saint Germain mnamo Desemba 2 2020.

Neymar aliishia kufunga mabao mawili huku Mashetani Wekundu wakikubali kichapo cha 3-1 katika mchezo ambao kiungo Fred alitolewa nje kwa kadi nyekundu.

Neymar kwa sasa anauguza jeraha ambalo limemaliza msimu wake.

Kama ilivyotajwa kwenye CBS Sports, Neymar alipata majeraha ya ACL alipokuwa kwenye majukumu ya kimataifa na Brazil na hivi karibuni alifanyiwa upasuaji. Sasa ameanza njia ya kupata nafuu na anatarajiwa kuwa nje ya uwanja kwa angalau miezi sita.