Timo Werner ampiku Antony wa Man Utd aliye na dakika 911 uwanjani bila bao wala asisti...

Timo Werner ambaye amekaa nje ya uwanja kwa miezi miwili alihitaji kucheza dakika 82 pekee ndani ya EPL ili kupata asisti, jambo ambalo Antony ambaye amecheza dakika 911 ameshindwa kufanya.

Muhtasari

• Bentancur alifunga chini ya dakika moja baada ya muda wa mapumziko, akipokea pasi kutoka kwa mchezaji Timo Werner kabla ya kupiga mpira na kumpita kipa Andre Onana

Antony na Werner.
Antony na Werner.
Image: Facebook

Fomu ya Winga wa Manchester United, Antony imerejelewa tena na kuwa gumzo mitansaoni baada ya mchezaji Timo Wwerner kumpiku kwa tija yake uwanjani baada ya kushiriki mechi moja tu.

Timo Werner ambaye amekuwa kwenye jeraha kwa kipindi cha miezi miwili iliyopita alinunuliwa kwa mkopo na Tottenhma Hostspurs na mechi yake ya kwanza kushiriki ilikuwa dhidi ya Manchester United ugani Old Trafford usiku wa Jumapili.

Werner alimbaye alitolewa kunako dakika ya 82 alipigiwa makofi baada ya kutoa asisti ya kupelekea bao la kusawazisha kunako mwanzo wa kipindi cha pili.

Hii ni kinyume na mwenzake Antony ambaye anacheza wingi pia ambaye ameshiriki dakika 911 bila kutoa asisti wala bao hala moja.

Katika mecho hiyo, Richarlison na Rodrigo Bentancur walifungia Spurs, iliyosalia nafasi ya tano kwenye jedwali, sawa na pointi 40 na Arsenal iliyo nafasi ya nne lakini ikiwa imecheza mchezo mmoja zaidi. United walipanda hadi nafasi ya saba, lakini wapo nyuma kwa pointi nane kutoka kwenye nafasi nne za juu.

United walianza vyema kwa bao la Rasmus Hojlund dakika ya tatu. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 20 alifunga kwa mara ya pili katika mechi nyingi za nyumbani kwa shuti kali la mguu wa kushoto hadi kona ya juu. Richarlison alitumia vyema alama mbovu za United na kufunga bao la kusawazisha kwa kichwa dakika ya 19.

Marcus Rashford aliirejesha United kileleni muda mfupi kabla ya mapumziko kwa bao moja-mbili la haraka na Hojlund likiwa ni bao lake la nne msimu huu.

Bentancur alifunga chini ya dakika moja baada ya muda wa mapumziko, akipokea pasi kutoka kwa mchezaji Timo Werner kabla ya kupiga mpira na kumpita kipa Andre Onana.